Jumatano , 14th Mei , 2014

Ommy Dimpoz, staa wa muziki wa Bongo ambaye kwa sasa yuko nchini Uingereza kwa ajili ya shughuli za kimuziki, amewataka mashabiki wake kuendelea kutarajia mabadiliko na burudani zaidi katika shoo zake

Ommy Dimpoz

Hii ni kutokana na jitihada zake za kujifunza kila siku mambo mapya ya kuboresha kazi yake anapokuwa jukwaani.

Ommy ambaye ni moja ya wasanii watakaotumbuiza katika jukwaa wakati wa ziara za muziki za Kili 2014 zitakazoanza tarehe 24 mwezi huu, amesema kuwa, amekuwa ni mtu wa kujifunza na kufanya mazoezi sana huku akipokea maoni ya watu kwa lengo la kuwasha moto zaidi jukwaani, na hapa anatupatia ripoti mwenyewe.