
Akizungumza na www.eatv.tv, Pilipili amesema alishona nguo hiyo kwa makusudi ili kutaka utofauti, na ndiye fundi anayemshonea nguo zake nyingi.
“'He is the best', anaweza kufanya nguo ambayo ikakustiri, lakini ikasababisha watu waizungumzie, mimi nimefurahi nimeipenda mno, hata valentine day nitavaa hii hii, lazima niwe na kitu ambacho ukikiona tu utazungumzia, ipo kama ninavyotaka mimi, amefanya vizuri”, amesema Mc Pilipili.
Nguo hiyo ya Mc Pilipili ilizua gumzo mtandaoni tangu siku ambayo alimvisha pete mchumba wake, Philomena Thadey maarufu 'Qute mena' huku akidhihakiwa kwa kufanana na mpishi, jambo ambalo mwenyewe amesema amelifurahia.