Jumanne , 6th Feb , 2024

CEO wa Next Level Music Rayvanny amekutana na mama mzazi na meneja wa staa wa muziki Africa Burna Boy ‘Bose Ogulu’ katika utolewaji wa tuzo za Grammy 2024 Los Angeles Marekani.

Picha ya Rayvanny na Mama Burna Boy

Rayvanny ameshea picha hii kwenye Insta Story yake akiandika 

“Mama ni mama, sikujua kama una upendo huo kwa muziki wa Tanzania”.

Rayvanny ni mmoja ya mastaa wa Africa walioshuhudia live tukio hilo la utolewaji wa tuzo kubwa za muziki duniani zilizofanyika mara 66 tangu kuanzishwa kwake.