
Akiwa nchini Senegal sambamba na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, Rihanna ameshiriki kwenye kongamano kubwa la kuchangia kuinua sekta ya elimu nchini humo, na kusema kwamba hawataacha kufanya hivyo mpaka pale watakapohakikisha kila mtoto anakwenda shule na kupata elimu bora.
“Haya ni mapambano ambayo hatutaacha kwamwe kupambana mpaka pale kila mtoto wa kiume na mtoto wa kike ana uwezo wa kupata elimu”, alisikika Rihanna akisema hivyo.
Kwa upande wa Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, amesema suala la kuchangia elimu sio la kujiamualia, ni suala nyeti na la loazima.
Kwenye mkutano huo uliofanyika Dakar nchini Senegal, Rihanna sambamba na Rais Emmanuel Macron wa Ufarsansa, waliwataka viongozi wa dunia na mashirika makubwa wanyotoa misaada kuongeza juhudi za kuinua elimu kwa nchi zinazoendelea barani Afrika.