Jumatatu , 11th Dec , 2017

Rapper Bonventure Kabogo maarufu kama Stamina anayeuwakilisha vyema mkoa wa Morogoro ,yuko mbioni kuachana na chama la ukapera baada ya kumvisha pete ya uchumba mpenzi wake wa muda mrefu.

Tukio hilo la kumvisha pete mpenzi wake limefanyika mkoani Morogoro ambapo ndio nyumbani kwao Stamina na baada ya tukio hilo wasanii wenzake  wampongeza kwa hatua hiyo na kumuomba asihishie hapo amuoe kabisa mpenzi  wake huyo.

Kupitia ukurasa wake wa instagram msanii mwenzake ambae wanafanya naye kazi kwa karibu hivi sasa Roma mkatoliki amemtahadharisha kwa kumwambia " Congratulation My Brother @staminashorwebwenzi On Your #Engagement .Im Proud Of You Son....Sasa #Umuoe Sio Uishie Kwenye #Pete Tu!!Nisaidieni #Kumuwish Mdogo Wangu Marafiki!!"