Alhamisi , 12th Nov , 2020

Msanii wa HipHop Bongo anayeishi nchini Marekani kwa sasa Roma Mkatoliki, ameiambia timu yake ya Simba waseme ukweli ili mashabiki wa timu hiyo wajiandae kisaikolojia kama mchezaji wao Clatous Chama atajiunga upande wa watani wao Yanga.

Kulia ni msanii Roma Mkatoliki, kushoto ni mchezaji Clatous Chama

Akifunguka hilo kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Twitter Roma Mkatoliki ameandika kuwa

"Kuliko kuturusha rusha roho na kutuweka roho juu, tuambieni moja tujue na kujiandaa kisaikolojia Chama anaenda Uto au bado tupo naye".

Kupitia kwenye mitandao ya kijamii kuna stori ambazo zinaendelea na zinasemakana kuwa huenda mchezaji huyo Raia wa Zambia akajiunga na mabingwa wa kihistoria hapa nchini Yanga SC.