Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waajiri wasiokata madeni ya HESLB kushitakiwa

Jumatatu , 19th Sep , 2016

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu imesisitiza waajiri wote nchini kuwakata pesa kwa ajili ya kulipa deni waajiri wote waliokopeshwa na bodi hiyo.

Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano Bwana Cosmas Mwaisobwa

Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano Bwana Cosmas Mwaisobwa ametoa msisitizo huo wkati akijibu maswali ya wananchi kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV, katika kipengele cha Kikaangoni,

Amesema kuwa suala hilo ni la matakwa ya kisheria hivyo hakuna muajiri yeyote anayepaswa kukwepa suala hilo, na kwamba endapo mwajiri atabainika kutokana deni hilo kutoka kwa waairiwa wake, atakumbana na mkono wa kisheria.

“Hili suala lipo kisheria, endapo mwajiri hatakata na kuwasilisha pesa hizo bodi ya mikopo anaweza kukumbana na faini, au hatua zaidi ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani” Alisema Mwaisobwa .

Aliongeza kuwa ili kuwabana waajiri wanaokwepa kukata madeni hayo, serikali kuanzia mwaka ujao wa fedha imeagiza wakaguzi wa mahesabu akiwemo Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kutopitisha hesabu za kampuni au taasisi yoyote ambazo hazitaonesha kukatwa kwa deni hilo.

“Kuanzia sasa ili hesabu zipitishwe, ni lazima tuone jinsi ambavyo madeni hayo yamekatwa, vinginevyo kampuni au taasisi inapata hati chafu, jambo ambalo lina madhara makubwa, kwahiyo ni bora waajiri wakajiepusha na mambo kama hayo”.

Alisema kiwango kinachopaswa kukatwa ni asilimia 8 ya mshahara wa mfanyakazi ambaye alikopshwa na bodi hiyo.

Mwaisobwa pia alionya waajiri wanaokata madeni hayo bila kuyawasilisha bodi ya mikopo, na kusema kuwa endapo watabainika watachukuliwa hatua za kisheria.

Kuhusu malalamiko ya baadhi ya watu kuandikiwa deni kubwa kuliko pesa waliyokopa, Mwaisobwa amesema kila mtu atalipa pesa ileile aliyokopeshwa, pamoja na asilimia 6 ambayo ni kiwango cha kulinda thamani ya fedha Value Retantion Fee), na endapo amechelewa kulipa, atatakiwa kulipa na fain ambayo ni asilimia 10 ya fedha aliyokopshwa wa mwaka.

Hadi sasa bodi hiyo imekwishakopesha kiasi cha takribani trilioni 2.44.

Fuatilia Kikaangoni kila Jumatano, saa 8:00 mchana.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea