Jumapili , 31st Mar , 2019

Mwanamke mmoja kutoka nchini Uingereza, aitwaye Amethyst Realm ameweka wazi kuwa amewahi kufanya mapenzi na zaidi ya mizimu 20.

Amethyst Realm.

Akizungumza katika Kipindi cha Televisheni cha 'This Morning' cha ITV ya Uingereza anasema kuwa kisa hicho kilianza Mwaka 2005 akiwa na miaka 15 ambapo yeye pamoja na familia yake walipohamia katika Nyumba mpya na baada ya siku chache akaanza kuhisi mtu anamshikashika usiku lakini hamuoni.

Hali hiyo ilipelekea hadi kufanya nae mapenzi, na iliendelea kumtokea kwa miaka mingi.

Anasema hali hiyo ilianza kama nguvu fulani hivi inayompapasa, baadaye akawa anaona kabisa anahemewa mihemo maeneo ya shingoni na kushikwashikwa sehemu za mwili wake usiku bila ya kumuona anayefanya hivyo na baadae wanafanya mapenzi.

Amethyst ameendelea kusimulia kuwa hali hiyo iliendelea hadi siku moja alipokwenda kwa mpenzi wake. Mpenzi wake alipokua akirudi nyumbani usiku alikutana na kivuli kinakimbia, hali iliyomfanya kuhisi kuwa mpenzi wake alikuwa akimsaliti na mwanaume mwingine ndani.

"Nilimwambia mpenzi wangu asihangaike kumfatilia kwasababu asingeweza kumpata kwakua hakua mtu wa kawaida bali ulikua ni mzimu, na baada ya kusema hayo akabeba mizigo yake akawa ameniacha", anasimulia Amethyst.

"Mzimu hauwezi nitoa out siwezi kwenda nao popote lakini raha niliyokuwa naipata sijawahi pata kwa mwanaume yeyote, nilikuwa na enjoy sana na ninapata usingizi mzuri naota ndoto nzuri pia, kuna muda nageuzwa style tofauti kabisa", ameongeza Amethyst .

"Wakati wa tendo nahisi miguso na raha ya ajabu huku anaenifanya simuoni na kuna muda hua nashangaa nageuzwa kabisa kufanyishwa mapenzi kwa staili tofauti tofauti" - Amethyst .

Amethyst amesema kuwa amefanya hivyo kwa muda mrefu sana na mizimu zaidi 20 tofauti na hadi alipobeba ujauzito Mwaka 2017 na aliridhia kuendelea na uhusiano mpaka mzimu huo ulipotoweka wenyewe.