Alhamisi , 5th Feb , 2026

Kuliko kufanya sherehe ya Milioni 50 kwa siku moja, bora tukajenge, hii ndiyo kauli inayozidi kushika kasi miongoni mwa wanaume wengi kwa sasa.

 
Utafiti mpya uliofanywa na mtandao wa masuala ya harusi wa ''The Knot'' umebaini kuwa takribani 90% ya wanaume kwa sasa wako tayari kufanya sherehe ndogo ya harusi (Small Wedding) au hata kuacha kabisa kuliko kufanya sherehe kubwa

Sababu kubwa iliyotajwa ni Uchumi, huku Wanaume wengi wameeleza kuwa wanapendelea kuepuka gharama kubwa za kumbi, vyakula, watu wengi na badala yake fedha hizo zitumike kama mtaji wa maisha yao ya baadaye.

Hapa kwetu sasa mambo ya ''ngoja nifunge mtaa leo'' au kauli ya ''nimechanga kwenye sherehe nyingi sana wacha na mimi wanichangie'' lakini wanaume wengi kwa sasa wanasema "Hapana, tufikirie kwanza maisha baada ya harusi''