Jumatatu , 25th Apr , 2022

Bibi wa miaka 70 Kamaliza Verena kutoka Rwanda anadai kwamba yeye bado ni bikira na hajakata tamaa ya kupata mume akisubiria miujiza ya Mungu.

Picha ya Bibi Kamaliza Verena

Bibi huyo anasema "Mimi bado ni bikira. Sijawahi kuolewa, sijawahi kulala na mwanaume na sijui inakuwaje. Bado nina matumaini ya kupata mpenzi".

Pia ameongeza kusema huenda hajapata mume kwa sababu ya maumbile yake ya kimo kifupi akieleza kuwa hana ujasiri wa kukaribia au kuzungumza na wanaume.