Jumanne , 17th Mar , 2020

Bilionea nchini China na muanzilishi wa kampuni ya Alibaba Jack Ma, amesema ana mpango wa kuchangia barakoa (Mask) na test kits katika Bara la Afrika kwa ajili ya kuchukua vipimo vya kujikinga dhidi ya Virusi vya Corona.

Bilionea wa China, Jack Ma

Bilionea huyo tayari amechangia upatikanaji wa vifaa Milioni 1 vya kupimia Corona, Barakoa milioni 6, mavazi elfu 60 ya kujikinga na ugonjwa huo pamoja na viziba uso.

Akitoa maelezo hayo ya kuchangia vifaa hivyo Jack Ma amesema "Kwa sasa wote tunaishi katika msitu mmoja ambao unawaka moto, haipaswi kwetu sisi kudharau, kuchukulia kawaida au ku-panic au kushindwa kuchukuliwa hatua ili kuwaachia Waafrika wapambane peke yao dhidi ya virushi hivi vya Corona".