Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Emmett Till alivyodhulumiwa uhai wake

Alhamisi , 18th Oct , 2018

Tahadhari, picha ya kuogopesha chini.

Emmett Louis Till alizaliwa Julai 25, 1941 huko Chicago nchini Marekani, akiwa mtoto wa mwanajeshi Louis Till aliyezaa na Mamie Elizabeth Till-Mobley.

Mtoto Emmett Till

Mnamo mwezi Augosti 1955, Emmett Till akiwa na umri wa miaka 14, alikwenda kutembelea ndugu zake huko Mississippi, siku moja alikwenda katika duka ambalo lilikuwa likimilikiwa na raia wa kizungu alyejulikana kwa jina la Bryant. Alipokwenda dukani alikutana na mke wa Bryant, Nicole, ambaye alikuwa akiuza duka hilo, kilichoendelea hakikujulikana lakini mwanamke huyo alimtuhumu kumdhalilisha kingono ikiwemo kumshika matiti.

Baada ya siku kupita mume wa Nicole, Roy Bryant na kaka yake J.W Millam, walimchukua Emmett kutoka nyumbani kwao, huku ndugu yake mmoja akishuhudia, walimchukua na kwenda naye mahali ambako walimpiga vibaya na kisha kumpiga risasi kichwani, wakamzungushia waya shingoni kisha wakamtupa kwenye mto  Tallahatchie.

Baada ya siku kupita mwili wa Emmet ulipatikana ukiwa umeharibiwa vibaya, ukarudishwa Chicago kwa mama yake ili kuendela na shughuli za mazishi, mama yake aliacha mwili wa mtoto wake ili watu waone jinsi alivyouawa kikatili na watu weupe.

Msiba wa Emmett ulihudhuriwa na watu wengi ikiwemo wanaharakati wa kutetea haki za watu weusi, ambao walikuwa wakinyanyaswa sana miaka ya nyuma huko nchini Marekani.

Baada ya hapo ilifunguliwa kesi dhidi ya waliohusika na tukio la kumuua Emmett, Roy Bryant na kaka yake J.W Millam, lakini watuhumiwa hao waliachwa huru.

Miaka ya hivi karibuni mwanamke aliyemtuhumu Emmet kuwa alimdhalilisha kwa kumshika matiti, Bi. Caroline Bryant, alinukuliwa akisema kwamba mtoto huyo hakuwahi kumfanyia hivyo kama alivyotoa ushahidi hapo awali, isipokuwa alidanganya tu na kushinikizwa.

Kifo cha Emmett kiliibua hisia kali kwa wanaharakati wa kutetea haki za watu weusi, hasa baada ya kushuhudia mwili wa Emmett jinsi ulivyojeruhiwa vibaya, na kubaki kama icon ya harakati za watu weusi nchini Marekani.                          

                             ​​​​​​

                                            Mwili wa Emmett ulivyojeruhiwa na wauaji wake

                 Mama yake Emmett akiaga mwili wa Emmet huku sanduku lake likiwa limeachwa wazi

       

               

                              Bi. Caroline Bryant ambaye alimtuhumu Emmett kumdhalilisha kingono

                                  

                                 Wazungu waliotuhumiwa kumuua Emmett, Roy Bryant na kaka yake J.W Millam

 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani