Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Meridian Bet yaendelea kutoa msaada kwa jamii

Jumatano , 20th Jan , 2021

Kampuni inayojihusisha na michezo ya kubahatisha ya Meridian Bet, imetoa msaada wa vitu mbalimbali kwa walemavu wanaosali katika kanisa la Waadiventista wasabato, Manzese Jijini Dar es Salaam.

Meneja Ustawi wa Kampuni ya Meridian Bet, Amani Maeda, akikabidhi msaada kwa mmoja wa walemavu jijini Dar es Salaam

Akizungumza wakati akitoa msaada huo Meneja Ustawi wa Kampuni hiyo Amani Maeda, amesema kuwa kampuni hiyo imejiwekea utaratibu wa kusaidia watu wenye uhitaji maalum ambapo leo wameamua kutoa msaada kwa taasisi hiyo.

"Huu ni mwendelezo wa kutoa msaada kwa watu wenye uhitaji maalum na hapa tumekuja na mchele, unga wa ugali, sukari, mafuta ya kupikia, pempas za wakubwa pamoja na miwani lakini mtatuambia changamoto mlizonazo ili kwenye mkono wa kugusa Jamii tuweze kuwafikia", amesema Amani Maeda.

Kwa upande wake mratibu wa walemavu hao Oloo Vincent, ameshukuru kwa msaada huo ambapo pia ametumia nafasi hiyo kuiomba serikali pamoja na jamii kwa ujumla kuwaunga mkono walemavu hao kwani pamoja na ulemavu walionao lakini wanajishughulisha na ushonaji wa viatu.

Nae Mwenyekiti wa walemavu hao Isdori Mrisho, ameishukuru kampuni hiyo kwa moyo wao wa utoaji na kuongeza  kuwa  watu wengi wana uwezo mzuri kiuchumi lakini hawana moyo wa utoaji.

Akizungumza kuhusiana na kuwakumbuka walemavu walioko vijijini, Katibu wa Walemavu hao Berdina Sailas, amesema kuwa asilimia kubwa ya walemavu wako vijijini na hawapati msaada kwa kuwa watu hawawafikii hivyo ameiomba kampuni ya Meridian Bet iangalie namna ya kuwafikia walemavu walioko vijijini.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala