Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Vitu 5 vya kuzingatia ukishanunua simu mpya

Jumanne , 1st Dec , 2020

Ukishanunua simu mpya, kila mmoja anakuwa na haraka ya kufungua boksi kuiwasha simu yake na kuanza kutumia, sasa hivi ni vitu 5 muhimu vya kuzingatia baada ya kununua simu mpya ( kwa leo tutaziangazia simu za Andoid )

Vitu 5 vya kuzingatia ukishanunua simu mpya

Angalia 'updates' mpya za Apps kwenye simu yako

Ukishaiwasha nenda kwenye mpangilio wa simu (settings), kisha nenda kwenye kuhusu simu (About device), kisha Software updates. Kufanya hivi inasaidia kuifanya simu kufanyakazi kwa ufanisi, kuimarisha ulinzi na kuongeza uimara.

Ondoa Apps ambazo huzihitaji

Hatua nyingine muhimu ni ya kuondoa Apps ambazo hazina umuhimu zinazokuja moja kwa moja kwenye simu ili kuongeza nafasi ya simu yako.

Nakili data zako kutoka kwenye simu ya awali

Ukiwa unaseti vitu vyako kwenye simu mpya, Androids itakuuliza wapi unataka kunakili (copy) taarifa zako kutoka kwenye kifaa cha zamani, ambapo unaweza kutumia USB cable inayoendana au kwa kutumia Apps za kuhamishia taarifa mbalimbali.

Angalia Apps za chaguo msingi (Default Apps)

Ziangalie 'Default Apps' kwenye simu yako na uzipangilie kwa namna unayotaka. Ili kuzipata ingia kwenye Mpangilio wa simu (settings), kisha Apps & Notifications, kisha Default Apps.

Wezesha kipengele cha kuitafuta simu yako ( Find my Device )

Huduma ya kutafuta simu yako kutoka Google itakuwezesha kuitafuta, kuifunga na kuizima kabisa pindi inapopotea, kwahiyo hakikisha unaiwezesha simu yako na huduma hii tangu siku ya kwanza.

Ili kuwezesha simu yako, nenda kwenye mpangilio wa simu (Settings), kisha ulinzi (Security), kisha tafuta kifaa changu (Find my Device) na kuwasha. Hakikisha ukiwa unafanya hivyo, umewasha data na 'location'.
 

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu