Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Azam FC yapata ahueni!

Ijumaa , 18th Aug , 2017

Uongozi wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC kupitia Afisa habari wao Jaffery Iddy Maganga amesema wameshamalizana na Kagera Sugar kuhusiana na sakata la Mbaraka Yusuph na sasa yupo huru kuitumikia Azam FC.

Maganga amebainisha hayo baada ya kuwepo mvutano wa muda mrefu kati ya Kagera Sugar na Azam FC ambapo kila timu ilikuwa inavutia upande wake, hatimaye mvutano huo umepata suluhisho.

"Jana tulifanya kikao na Kagera Sugar na mwisho tumefikia muafaka kuhusiana na suala hilo na sasa Mbaraka ni mchezaji halali wa Azam FC. Lakini bado hatujaanza kumtumia kwa sababu aliumia akiwa na timu ya Taifa hivyo bado yupo chini ya uangalizi wa daktari na anafanya mazoezi mepesi mepesi ili baadaye aweze kujiunga na kikosi kwa ajili ya mechi za Ligi" alisema Maganga.

Mshambuliaji Mbaraka Yusuph.

Pamoja na hayo, Maganga amesema timu ya Kagera Sugar  wametoa barua maalum ya kumuachia Mbaraka aitumikie Azam FC kwa sasa.

Mbaraka Yusuph amesaini kandarasi ya miaka miwili kuwatumikia wanarambaramba hao wa Vingunguti.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea