
Azpilicueta 32, ametoa kauli hiyo baada ya sare ya magoli 3-3 ugenini dhidi ya Zenit St Petersburg ya Urusi huku kwenye michezo miwili mpaka sasa wakiruhusu magoli sita kwenye lango lao.
"tumekuwa imara siku zote, ndio maana haturuhusu nafasi au magoli mengi kwa wapinzani lakini kwenye michezo miwili iliyopita tumeruhusu magoli sita na kwetu sio jambo jema ,tunapaswa kulitatua jambo hili” Azpilicueta amesema
Chelsea imemaliza nafasi ya pili nyuma ya Juventus kwenye kundi H ilhali ni ya tatu kwenye msimamo wa Epl huku Jumamosi watakuwa Stamford Bridge wakiwakaribisha Leeds United ya mwalimu Marcelo Bielsa.