Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Baada ya ubingwa, Kocha Mchenga amzuia Baraka

Ijumaa , 11th Oct , 2019

Kocha wa Mchenga Bball Kings ambao ni mabingwa wa michuano ya Sprite Bball Kings 2019, Mohamed Yussuf 'Mudi' amesema kuwa wapinzani wasitarajie kuwa staa wa timu hiyo Baraka Sadick anaweza kuondoka.

Kocha wa Mchenga (wa kwanza kushoto), MVP Baraka Sadick (wa tatu kutoka kulia) wakiwa na baadhi ya mashabiki

Ameyasema hayo katika kipindi cha Dadaz kinachoruka kupitia EATV, ambapo amesema kuwa anamfahamu vizuri Baraka Sadick tangu akiwa kijana mdogo kipindi alipokuwa akija katika mazoezi yake.

"Awali kabisa wakati mimi nacheza kikapu, wao (Baraka na wenzake) walikuwa wanakuja wakiwa wadogo wananiona nacheza, tukishamaliza na wao wanaingia uwanjani wanarusha mipira. Nimekuwa mfano bora kwake, simaanishi nimehusika asilimia 100 lakini nimemfundisha", amesema Mudi.

"Kina Baraka hawawezi kuondoka Mchenga kwa sababu mimi nipo, hiyo ipo hata kwa Tamaduni kuna watu wa aina hiyo, mfano yule Stefano wa Tamaduni niliwahi kumfuata akaniambia subiri baada ya wiki na hatimaye siku zikapita nyingi mwisho akaniambia siwezi kuacha hapa na mimi nikamuelewa", ameongeza.

Akizungumzia ushindani aliokutana nao dhidi ya Taamaduni na fainali ngumu kwake, Mudi amesema, "katika game za fainali mwaka huu dhidi ya Tamaduni, game ya kwanza ndiyo ilikuwa hatari zaidi kwetu, walikuwa na nafasi ya kushinda. Tulikuwa tukiwazidi wanarudisha ilikuwa ngumu sana".

Mchenga wameshinda ubingwa baada ya kushinda michezo mitatu ya fainali dhidi ya Tamaduni, na kujishindia kitita cha Sh. milioni 10 na Tamaduni wakijishindia Sh. milioni 3. Mchezaji Baraka Sadick ameshinda tuzo ya MVP kwa msimu wa pili mfululizo na kujishindia Sh. milioni 2.

 

HABARI ZAIDI

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria