Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Barcelona yaongoza duniani kwa wafuasi mtandaoni

Alhamisi , 23rd Jan , 2020

Mtandao unaojihusisha na masuala ya data na fursa za kimtandao kwa wanamichezo, vilabu na mashirikisho wa 'Result Sports' wenye makao makuu mjini Büdingen nchini Ujerumani umetoa listi ya klabu za soka zenye wafuasi wengi duniani katika mtandao ya kijamii.

Wachezaji wa Barcelona na Simba

Data hizo zilizotolewa mwezi Januari 2020 zinaonesha kuwa Barcelona inaongoza duniani kuwa na wafuasi wengi kwenye mitandao ya kijamii, ikiwa na wafuasi zaidi ya milioni 260 kutoka katika mitandao yake ya Instagram, Twitter, Facebook, YouTube na milioni 8 kutoka mitandao mingine.

Real Madrid inakamata namba mbili ikiwa na wafuasi zaidi ya milioni 258, Manchester United ikishika namba tatu ikiwa na wafuasi zaidi ya milioni 142. Chelsea ina wafuasi zaidi ya milioni 93 katika nafasi ya nne huku Juventus ikishika namba tano kwa wafuasi zaidi ya miloni 90, nafasi ya sita ni Bayern Munich, Liverpool nafasi ya saba, PSG nafasi ya nane, Man City nafasi ya tisa na Arsenal nafasi ya 10.

Kwa klabu za Afrika, mabingwa mara nane wa michuano ya Klabu Bingwa Afrika Al-Ahly inaongoza kwa wafuasi wengi ikiwa na zaidi ya wafuatiliaji milioni 25, ikishika namba 18 duniani. Nafasi ya pili kwa Afrika inafuatiwa na Zamalek iliyo na wafuasi zaidi ya milioni 11 huku ikishika nafasi ya 32 duniani.

Kwa Afrika Mashariki inaongozwa na klabu ya Simba ambayo imeingia kwa mara ya kwanza katika listi hiyo, ambayo imeshika nafasi ya 151 duniani huku ikiwa na wafuasi zaidi ya milioni moja. Facabook ina wafuasi zaidi ya 568,000, Instagram ikiwa na wafuasi zaidi ya milioni 1, Twitter ina wafuasi takribani 142,000 na YouTube ikiwa na wafuasi zaidi ya 21,000.

 

HABARI ZAIDI

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera