Vivier Bahati-Kocha msaidizi wa Azam
Kauli ya Koch huyo raia wa Burundi inakuja kufuatia baadhi ya wakosoaji kudai kuwa kukosekana kwa nyota hao waandamizi kumechangia kwa asimilia kubwa Azam kupoteza mchezo wao wa Ligi Kuu Tanzania bara dhidi ya Yanga ambao wana lambalamba walinyukwa bao 2-0 siku ya Jumamosi.
Akizungumzia hilo, Bahati amesema''Hata wangekuwepo wachezaji hao kipigo tusingekikwepa, bahati mbaya wachezaji wetu hawakuwa katika hali ya nzuri, na Yanga walikuwa bora zaidi yetu''. Vivier Bahati.
Ikumbukwe Azam Fc ipo katika nafasi ya 11 katika msimamo wakiwa na alama 4 katika mechi 4 waliyocheza na hawajawa na matokeo mazuri msimu huu licha ya kufanya usajili mkubwa wa wachezaji.
Ikumbukwe Morris, Mudathir na Morris walisimamishwa kutokana na masuala bila kikomo kufuatia masuala ya utovu wa nidhamu.




.jpg?itok=5cvL0YaP)

