Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Chaneta kubebwa kwa mbeleko

Ijumaa , 20th Mei , 2022

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi Pauline Gekul amesema kuwa Serikali itaendelea kuvibeba vyama vya michezo ikiwamo CHANETA kwa mbeleko mbili, moja ikiwa yake na ya pili ikiwa ya Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha michezo inaimarika nchini.

viongozi wa chama cha netiboli Tanzania.

Kauli hiyo ya serikali imetolewa na Naibu Waziri Gekul Mei 20, 2022 akiwa njiani akitokea Babati mkoani Manyara kuja Dodoma kuendelea na shughuli zake za kikazi ikiwamo kufanya kikao na CHANETA ambacho ni Chama cha Mpira wa Netiboli nchini.

“Ninaposema mbeleko maana yangu kuwa mtoto anabebwa kwa ubeleko mmoja lakini pale kunapokuwa hakuna budi mama hufanya upendeleo wa kumbeba mtoto wake kwa mbeleko mbili kuhakikisha anafika mbali zaidi.”

Aliongeza kuwa yeye kwa ushirikiana na Waziri wake Mheshimiwa Mohammed Mchengerwa ubeleko wake umefungwa vizuri na vyama vya michezo vinakuwa imara na michezo inazidi kufanikiwa na ndiyo maana wamejiwekea utaratibu wa kukutana na vyama mbalimbali vya michezo kila mara.

“Ubeleko wa Rais Samia Suluhu Hassan katika michezo umekuwa imara zaidi kwa kuongeza bajeti ya michezo kila uchao.”

CHANETA wakiongoza na mwenyekiti wao Dkt. Devota Marwa wapo jijini Dodoma kwa ratiba maalumu ya mazungumzo ya kina na Serikali ambapo kwanza wameanzia na Bungeni ambapo walizungumza na wabunge wakiongozwa na watumishi kadhaa wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Wanatarajia kufanya kikao kizito na Naibu Waziri Gekul, ambapo CHANETA wanasema kuwa wamejindaa vema kuuboresha mchezo huo hapa nchini.

“Tumekamilika, uongozi wetu upo imara, tunahakika katika kikao hicho na serikali tutayaweka wazi mambo yetu kadhaa, tuna imani yatapokelewa kwa mikono miwili na mara zote Serikali imekuwa ikifanya hivyo.”

Katika kikao hicho CHANETA inaongozwa na viongozi wake 11 inayowajumuisha wanahabari wawili maarufu nchini Bi Shy-Rose Bhanji na Bi Betty Mkwasa.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa