
Novak Djokovic akishangilia ushindi
Kinara huyo kwenye viwango vya ubora Duniani amefuzu nusu fainali baada ya kumnyuka Matteo Berrettini kwa seti 5-7, 6-2,6-2,6-3 .
Zverev ambaye anashikilia nafasi ya nne kwenye viwango vya ubora Duniani ndiye aliyeizima ndoto ya Djokovic katika michuano ya Olimpiki baada ya kumtupa nje katika nusu fainali.
Iwapo Djokovic atashinda US Open atakamilisha kibindoni Grand Slam nne baada ya kufanikiwa kutwaa Australian Open, French Open na Wimbledon mapema mwaka huu.