Steven Gerrard
Gerrard alilaumu safu ya ulinzi kwa kuruhusu bao la kwanza kutokana na uzembe wa kawaida, na kipa Alisson Becker kwa kuanzisha shambulio la bao la pili. Hakukubaliana na madai ya mashabiki kuhusu faulo dhidi ya Virgil van Dijk kabla ya bao la kwanza, akisisitiza kuwa Van Dijk alipaswa kuwa imara zaidi.
Pia, Gerrard amemtaka kocha Arne Slot kumpa mshambuliaji chipukizi Rio Ngumoha nafasi ya kuanza mechi, akimkataa Gakpo kwa kudai Ngumoha anaweza kufanya vizuri zaidi yake
Msimu huu, Liverpool wamepoteza michezo mitano kutokana na mabao ya dakika za mwisho, hali inayowapa presha kubwa katika mbio za kumaliza ndani ya tano bora, huku Chelsea wakiwa na nafasi ya kuipiku timu hiyo endapo watashinda dhidi ya Aston Villa .


