Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kinachomvutia Gnako kwenye Sprite Bball Kings 2019

Ijumaa , 16th Aug , 2019

Msanii wa kundi la Weusi, Gnako 'Warawara', leo amefunguka kitu kinachomvutia kwenye msimu huu wa mashindano ya Sprite Bball King's ambayo yameandaliwa na East Africa Television na East Africa Radio kwa kushirikiana na kinywaji cha Sprite.

Msanii wa Weusi, Gnako

Akizungumza na  EATV & EA Radio Digital, Gnako amesema amefarijika na maandalizi ya msimu huu na yeye ni miongoni mwa wafuatiliaji wazuri wa mchezo wa mpira wa kikapu na amehudhuria mechi nyingi za mchezo huo lakini ameeleza masikitiko yake juu ya kutelekezwa kwa vipaji vinavyozalishwa.

"Nafuatilia sana mchezo wa 'Basketball', nilishapata bahati ya kwenda kwenye mashindano navutiwa kuona kama kuna vipaji, isipokuwa kinachoniumiza baadaye vile vipaji vinakuwa havina muendelezo baada ya kufanyika mashindano", amesema Gnako.

Aidha msanii huyo ameendelea kueleza kwamba "nafikiri kitu kizuri kiwepo baada ya mashindano ya Sprite Bball Kings,  bora kungekuwa na ligi au vitu ambavyo vinakuwa vinaendelea kutokea baada ya mashindano kwa sababu vipaji vikishapatikana vinakuwa vinaeleaelea". 

Ufunguzi wa mashindano hayo utafanyika kesho Jumamosi katika viwanja vya Mlimani City, Dar es salaam ambapo pamoja na mambo mengine kutakuwa na usajili wa timu shiriki katika michuano hiyo. Kamati ya mashindano inazialika timu zote nchini kuja kujiandikisha ambapo umri wa wachezaji ni kuazia miaka 16 na kila timu itaruhusiwa kuwa na wachezaji 10.

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi