
Lady Jay Dee
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Jay Dee amesema kuwa kutokana na kutokuwa na pesa ya kurekodi wimbo wake katika studio za MJ Records, alipata ofa ya kurekodi wimbo baada ya kushinda shindano la vipaji halisi.
Shindano hilo lilikuwa likirushwa na Radio One Stereo, ambapo kwa kipindi hicho mtu alikuwa akipigiwa simu na kisha ku'rap' au kuimba ili kuonesha kipaji chake.
Nilipata offer ya kurekodi wimbo wa kwanza baada ya kushinda shindano la Vipaji Halisi. Unapiga simu Radio One Stereo unaimba au ku rap kipindi “DJ Show” na Mike Mhagama . Na hapo ndio niliposikika rasmi , sikuwa na pesa ya Studio ya kumlipa Master Jay.
— Lady JayDee (@JideJaydee) January 25, 2019
Lady Jay Dee amefanikiwa kudumu katika muziki wa Bongo Fleva kwa miaka takribani 20, akidumu na ufundi wake ule ule. Ametoa jumla ya albamu 7 mpaka sasa, ambazo ni Machozi (2000), Binti (2003), Moto (2005), Shukrani (2007), The Best of Lady Jaydee (2012), Nothing But The Truth (2013) pamoja na Woman (2017).