Jumapili , 3rd Oct , 2021

Klabu ya Simba SC imethibitisha kuwa nyota wake Kibu Denis amemaliza utata wa uraia wake na sasa ameruhusiwa kuichezea klabu hiyo pamoja na timu ya taifa ya Tanzania ( Taifa Stars ).

Mchezaji Kibu Denis

Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, Simba SC ambayo imemsajili Kibu Denis katika dirisha kubwa la usajili kabla ya kuanza msimu huu akitokea Mbeya City imethibitisha kumaliza sakata hilo.

Kabla ya kujiunga na Simba SC, Kibu Denis ameshawahi kucheza katika madaraja mbalimbali ya soka nchini ikiwa Ligi daraja la tatu, Daraja la kwanza na ligi kuu.