Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kigoma yatinga Nusu Fainali Copa Coca Cola

Alhamisi , 18th Dec , 2014

TIMU ya Vijana ya Mkoa wa Kigoma imefanikiwa kutinga hatua ya Nusu Fainali baada ya kuishinda timu kutoka mkoa wa Mwanza katika michuano ya Copa Coca Cola ngazi ya Taifa iliyochezwa leo uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.

Akizungumza na East Africa Radio, Kocha wa Timu ya Mkoa wa Kigoma, Hamis Mabo amesema vijana wake walitumia sehemu ya makosa ya wapinzani wao hivyo kufanikiwa kuibuka na ushindi wa Goli 1-0.

Mabo amesema hatua waliyoifikia katika michuano hiyo ni nzuri hivyo wanategemea kuendelea kufanya vizuri zaidi na hatimaye kuibuka na ushindi.

Kwa upande wake kocha kutoka Timu ya mkoa wa Mwanza, Ahamed Simba amesema kushinda na kushindwa ni sehemu ya mchezo, hivyo kwa hatua waliyoifikia sio mbaya sana kwani ameweza kutambua makosa yaliyopo katika timu yake hivyo anayo nafasi kubwa ya kuweza kuyarekebisha.

Katika mchezo mwingine uliochezwa Uwanja wa Tanganyika Parkers jijini Dar es salaam, Timu ya vijana kutoka mkoa wa Morogoro imeondolewa katika michuano hiyo baada ya kufungwa na timu ya vijana kutoka mkoa wa Dodoma baada ya kufugwa goli 2-1 na kupelekea timu kutoka mkoa wa Dodoma kutinga hatua ya Nusu Fainali katika michuano hiyo.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu