Jumatatu , 10th Apr , 2017

Kocha wa zamani wa vilabu vya Simba ya Tanzania, Gor Mahia na AFC Leopard za Kenya Zdravko Logarusic amevunja mkataba na klabu ya ligi kuu ya Ghana, Asante Kotoko.

Kocha Zdravko Logarusic

Kotoko wamethibitisha kuwa wamevunja mkataba na Mcroatia, huyo, kwa makubaliano, baada ya kumpa kibarua, kilichodumu kwa miezi mitatu tu.

Siku za hivi karibuni, Loga alizuiliwa na mashabiki wa timu hiyo, kuendesha mazoezi kwa madai ya  kutoridhishwa na mbinu za kocha huyo, kufuatia timu kutoka sare na Inter Allies.

Loga aliiongoza klabu hiyo ya Ghana kwa michezo 11, ambapo alishinda michezo mitano, aka droo minne na kupoteza miwili.