Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kuhusu ligi kuchezwa kituo 1,klabu yamuomba Waziri

Jumanne , 26th Mei , 2020

Baadhi ya klabu za Ligi Kuu Tanzania bara zimeonekana kulalamikia gharama zitakazojitokeza pindi ligi itakapoendelea kwa kuchezwa katika kituo kimoja cha Dar es Salaam.

Mchezo wa Ruvu Shooting dhidi ya Simba

Hatua hiyo inakuja kufuatia Rais Magufuli kutoa ruhusa ya ligi kurejea na siku kadhaa baadaye Waziri wa Sanaa, Habari, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe kutoa utaratibu wa namna ligi itachezwa, akiitaja Dar es Salaam kuwa ni mkoa kwa ajili ya Ligi Kuu.

Afisa Habari wa Ruvu Shooting, Masau Bwire ni miongoni mwa waliotoa maoni yao katika hatua hiyo ambapo amesema kuwa utaratibu wa kucheza ligi katika kituo kimoja utaziathiri zaidi klabu za mikoani kiuchumi kutokana na gharama za kuweka kambi kwa mwezi mmoja.

Masau Bwire amesema gharama ya kuweka kambi katika hoteli kwa timu moja kwa mwezi mzima siyo chini ya Sh. milioni 58 kwa mwezi mzima, jambo ambalo si rahisi kwa klabu nyingi hasa za nje ya Dar es Salaam, hivyo amemuomba Mhe. Waziri kukaa na wadau kuweka utaratibu mzuri kwa klabu hizo.

Mapema kabla ya ruhusa ya kuendelea ligi kutolewa na Rais Magufuli, klabu ya Ndanda ililalamika kukosa pesa za kuendesha klabu hasa kutokana na madhara ya COVID-19 na kuiomba Bodi ya Ligi na TFF kutoa msaada, na baadaye Bodi ya Ligi ilijibu kuwa haina pesa za kuzisaidia klabu na badala yake wataziwahisha pesa za wadahamini wao.

HABARI ZAIDI

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera