
Mshambuliaji wa timu ay taifa ya Poland, Roberto Lewandowski.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 32, aliumia katika mchezo uliopita dhidi ya Andora ambao licha ya kufanyiwa mabadiliko alikuwa ameshaifungia nchi yake mabao mawili.
Lewandowski ambaye ameshaifungia Bayern Munich bao 42 katika michezo 36 ya mashindano yote msimu huu, anatarajiwa kuwa nje ya uwanja wa takribani siku kumi kuuguza jeraha hilo.
Nyota huyo atarejea nchini Ujerumani ambapo ataendelea kupata matibabu kabla ya kurejea dimbani.