Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manara azitaka pointi 6 za Mwanza, Mbao FC wajibu

Jumatano , 15th Jan , 2020

Kuelekea mchezo wa Ligi kuu soka Tanzania Bara kesho Alhamis 16, 2020, klabu ya soka ya Mbao FC imesema imejiandaa vizuri licha ya wapinzani wao Simba kuwa na kila kitu kinachoweza kuwapa ushindi.

Kushoto ni Haji Manara na kulia ni wachezaji wa Mbao FC

Akiongea na EATV & EA Radio Digital, kocha msaidizi wa Mbao FC Abdulmutik Hajji ameweka wazi kuwa wamefanya maandalizi yao vizuri kwa kuzingatia ubora wa wapinzani wao.

'Tumejiandaa vizuri kuelekea mchezo wa ligi kuu kesho dhidi ya Simba lakini tunaiheshimu Simba kutokana na uzoefu mkubwa ilionao', amesema Hajji.

Kwa upande wa msemaji wa Simba Haji Manara amesema wanataka kupata pointi zote 6 za michezo miwili ya Mwanza ambayo ni dhidi ya Mbao FC na Alliance FC.

'Sasa akili yetu tuelekeze Mwanza katika mechi mbili ngumu zijazo, tushirikiane kupata pointi sita za CCM Kirumba, Insha'Allah tutafanikiwa', ameandika Manara.

Msimu huu Mbao FC wamecheza mechi 16 ambapo wameshinda mechi 4, Sare 6 na kufungwa mechi 6, wakati Simba wamecheza mechi 14, wameshinda 11, sare 2 na kufungwa 1.

Katika dirisha dogo la usajili Mbao FC wamesajili wachezaji watatu ambao Omary Wayne kutoka Ndanda SC walinzi Hussein Iddi kutoka Mtibwa Sugar na Mackyada Franco kutoka Coastal Union.

Simba wao wamesajili mchezaji mmoja ambaye ni Luis Miquissone kutoka UD Songo ya Msumbiji.
 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani