Alhamisi , 20th Mar , 2014

Uongozi wa mabingwa watetezi wa ligi kuu ya soka Tanzania Yanga, umewataka mashabiki wa timu hiyo kuwa wavumilivu na kuipa sapoti kubwa timu hiyo katika kipindi hiki ambacho timu hiyo iko katika vita ya kutetea ubingwa wake huo.

Katibu mkuu wa timu hiyo, Beno Njovu amesema kuwa matokeo ya sare ya bao 1-1 katika mchezo wa jana dhidi ya Azam fc ni moja kati ya matokeo matatu katika mchezo wa soka, na pia ikumbukwe hata wapinzani nao wanakua wamejiandaa

Njovu amesema kuwa wana uhakika wakutetea kombe hilo na kuwataka mashabiki wa timu hiyo wawape moyo wachezaji ili wakaibuke na ushindi ugenini jumamosi hii dhidi ya maafande wa Rhino ya Tabora mchezo utakaopigwa katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi.