
Bondia Thomas Mashali
Mashali amesema, Chimwemwe siyo bondia mbaya na anajipanga vizuri kwa ajili ya mpambano huo kwani mpambano wowote wa ngumi hautabiriki hivyo anaamini maandalizi yake ya safari hii yatasaidia kuweza kuwafurahisha mashabiki wake na Watanzania kwa ujumla.
Mashali amesema, Chimwemwe ni bondia ambaye anafanya vizuri katika kazi zake na huwa anapambana kuhakikisha anaibuka na ushindi lakini kwa safari hii atahakikisha anafanya maandalizi ya kutosha ili kujihakikishia ushindi mbele ya mpinzani wake huyo.
Pambano hilo litapigwa mwezi wa Desemba mwaka huu jijini Dar es salaam.