Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mbadala wa Clatous Chama apatikana Simba SC

Alhamisi , 14th Oct , 2021

Kocha Msaidizi wa kikosi cha Simba, Mrwanda Hitimana Thierry amesema mchezaji mbadala wa kutengeneza nafasi za mabao klabuni hapo tayari ameshapatikana baada ya Chama kuondoka na wana matarajio makubwa kuwa atafanya vizuri.

Kocha Msaidizi wa Simba, Hitimana Thierry akiwa anasimami mazoezi.

Hitimana ameyasema hayo wakati akizungumzia maandalizi ya mchezo wa kuwania kufuzu hatua ya makundi michuano ya klabu bingwa Afrika ambapo Simba itacheza Jmapili 17, 2021 dhidi ya Jwaneng Galaxy nchini Botswana.

Hitimana amesema, “Katika hizi mechi ambazo tumecheza tumeona jinsi gani tulikuwa tukitengeneza nafasi na kushindwa kuzitumia, lakini mtu wa kutengeneza nafasi ya mwisho, tayari yupo mtu ambaye amepewa jukumu hilo na kuna matarajio makubwa ya kufanya vizuri kwenye mchezo wetu huu"

Maelezo ya Hitimana hayakutaja kwa jina mchezaji huyo mwenye majukumu hayo mapya lakini ripoti za kikachero zinaripoti kuwa ni miongoni mwa kiungo fundi, Larry Bwalya, winga Bernanrd Morrison na Pape Ousmane Sakho. Ikumbukwe kuwa Chama alikuwa kinara wa kutengeneza nafasi za mabao 'Assits' wa Ligi kuu msimu ulioisha 2020-21 kwa kutengeneza nafasi 15 na hata msimu juzi 2019-20 alitoa assist 8 na kuwa kinara katika VPL.

Msimu uliopita Bwalya alikuwa na assist 5 na Bernard Morrison alikuwa na assist 4 licha ya kukosa utulivu na kuwa na ingia toka kwenye kikosi cha kwanza ilhali Sakho alikuwa mchezaji bora wa Lgi kuu ya Senegel.

Kwa upande mwingine amegusia mazingira ya nchini Botswana ambayo wanajiandaa kukabiliana nayo.

“Tumejiandaa vizuri kimbinu na kiufundi, pia tumeshajua tutaenda kucheza kwenye joto kali, tumeanza kulifanyia kazi hilo na kuzoea hali hiyo kabla ya kuondoka kuelekea Botswana". Amesema Hitimana.

Simba inataraji kuondoka nchini Tanzania Ijumaa ya 18, 2021 kuelekea nchini Botswana kwa ajili ya mchezo huo.

HABARI ZAIDI

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera