Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Meneja aeleza hasara ya Simba kutolewa Kimataifa

Jumatatu , 9th Sep , 2019

Meneja wa klabu ya Simba, Patrick Rweyemamu amesema kuwa klabu yake imepata hasara kwa kiasi chake baada ya kuondolewa katika hatua ya awali ya Klabu Bingwa Afrika.

Patrick Rweyemamu

Ameyasema hayo katika mazoezi ya timu hiyo yanayoendelea Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujiandaa na ratiba ya Ligi Kuu Tanzania bara (VPL).

Rweyemamu amesema kuwa hasara inaweza kuwepo au isiwepo kwa klabu hiyo kutokana na namna uwekezaji ulivyofanyika, ambapo amebainisha kuwa uwekezaji mkubwa ulikuwa katika usajili pamoja na gharama za uwekezaji.

"Gharama inaweza ikawepo au isiwepo kwa sababu msimu uliopita tulikuwa tunasafiri, posho, bonasi, visa pamoja na mahitaji mengine", amesema Rweyemamu.

"Kwa upande mwingine tumepoteza hela pia, tulikuwa tunategemea kule kama chanzo cha mapato kwa sababu tulipofika robo fainali tulipata zaidi ya  Dolla laki 6 na elfu 50 kwahiyo nao ulikuwa ni mtaji kwetu na sasa hatutoupata. Ni changamoto lakini lazima tupambane", ameongeza.

Simba ilitolewa katika hatua ya awali ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika na klabu ya UD du Songo ya Msumbiji baada ya kutoka sare ya kufungana bao moja kwa moja katika uwanja wa taifa Jijini Dar es Salaam, ambapo katika mchezo wa kwanza nchini Msumbiji timu hizo zilitoka suluhu ya bila kufungana.

HABARI ZAIDI

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera