Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Messi sasa awa kinara wa Ballon d'Or

Jumanne , 3rd Dec , 2019

Usiku wa kuamia leo Desemba 3, 2019, jijini Paris Ufaransa zilitolewa tuzo za Ballon d'Or, ambapo katika tuzo ya mchezaji bora, mshindi aliibuka nyota wa Barcelona na Argentina Lionel Messi.

Messi akiwa na tuzo zake 6 za Ballon d'Or

Nyota huyo alitangazwa mshindi na mshereheshaji wa tuzo hizo ambaye alikuwa mshambuliaji wa zamani wa Chelsea na Ivory Coast Didier Drogba, hivyo kumfanya Messi afikishe tuzo 6 za Ballon d'Or na kuwa mchezaji mwenye tuzo hizo nyingi zaidi.

Katika kuwania tuzo hiyo Messi alikuwa anashindana na mpinzani wake wa muda mrefu Cristiano Ronaldo ambaye ni mshindi mara tano wa tuzo hiyo, pamoja na mlinzi wa Liverpool na Uholanzi Virgil van Dijk.

Miaka ambayo Messi ameshinda tuzo hiyo ni kuanzia mwaka 2009, ambapo alishinda mara 4 mfululizo hadi mwaka 2012, aliposimamishwa na Ronaldo ambaye alibeba 2013 na 2014 kabla ya Messi tena kushinda 2015.

Mwaka 2016 na 2017 Ronaldo akashinda tena na mwaka 2018 kwa mara ya kwanza tuzo hiyo ikaenda nje ya wachezaji hao wawili katika kipindi cha miaka 10, ambapo kiungo wa Real Madrid na Croatia Luka Modric alitwaa.

Mwaka 2019 Messi ameshinda tena tuzo hiyo, ambapo imeelezwa kuwa amesaidiwa na takwimu zake binafsi kutonana na timu yake ya Barcelona kushinda taji la La Liga pekee huku yeye binafsi akiibuka mfungaji bora barani Ulaya.

Katika tuzo hizo, mchezaji bora kijana chini ya miaka 21 ni Matthijs de Ligt wa Juventus ambaye alikuwa na mwaka mzuri akiwa na Ajax na Uholanzi. Golikipa bora alikuwa ni Alisson Becker wa Liverpool na Brazil.
 

HABARI ZAIDI

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita