Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mhilu amesema yupo tayari kurejea Yanga.

Jumanne , 30th Jun , 2020

Yusuph Mhilu amesema yupo tayari kujiunga na waajiri wake wa zamani klabu ya Yanga iwapo watapeleka ofa itakayokubalika kwa pande zote mbili.

Mshambuliaji machachari wa Kagera ,Sugar Yusuph Mhilu katika picha,wakati akisaini mkataba wa kuitumikia miamba hiyo ya mkoani Kagera.

Mshambuliaji wa klabu ya Kagera Sugar,inayoshiriki ligi kuu ya soka Tanzania bara,Yusuph Mhilu ameifungulia mlango klabu yake ya Zamani ya Yanga,iwapo itahitaji huduma yake kwa mara nyingine.

Nyota huyoa ambaye ndiye kinara wa mabao kwa wachezaji wazawa katika ligi kuu Tanzania bara akiwa na mabao 13,amesema amesikia taarifa za kuhitajika na Yanga ingawa bado hajapokea barua rasmi ambayo anasisitiza kwamba hatosita kurejea mitaa ya Twiga na Jangwani kama nafasi itapatikana.

Mhilu ambaye alilelewa katika klabu ya Yanga ya vijana kwa miaka mitatu,na kupewa nafasi katika kikosi cha wakubwa na aliyekua kocha wa klabu hiyo Mwinyi Zahera,alishindwa kuendelea kuaminiwa baada ya kupelekwa kwa mkopo katika klabu ya Ndanda mnamo msimu wa mwaka 2018/19 kabla ya kujiunga na Kagera msimu huu.

Ndani ya msimu huu ,Mhilu amehusika katika mabao 17 ya Kagera Sugar ambapo amefunga 13 na kutoa pasi za mabao 4,na sasa ndiye mfungaji bora wa pili katika ligi kuu nyuma ya kinara Meddie Kagere wa Simba mwenye mabao 19 hadi sasa.

Hakuna mchezaji wa klabu ya Yanga ambaye amefikisha idadi ya Mhilu kiasi cha kuwafanya mabosi wake wa zamani kufikiria kumrejesha nyota huyo wa kitanzania.

Katika hatua nyingine mhilu amewashauri Yanga kuwa watulivu katika kipindi hiki wanachopitia huku akiamini wakijipanga wanaweza kurejesha makali yao waliyokua nayo kwa misimu kadhaa iliyopita

HABARI ZAIDI

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya