Alhamisi , 13th Oct , 2016

Vilabu vya mchezo wa mieleka nchini vimetakiwa kujipanga kwa ajili ya kufunga kalenda ya mwaka huu na kuanza msimu mpya kwa kuonesha changamoto ya kiushindani katika mashindano mbalimbali ya ndani na nje ya nchi.

Andrew Kapelela - Mwenyekiti wa Chama cha Mieleka nchini AWATA

Mwenyekiti wa Chama cha Mieleka nchini AWATA Andrew Kapelela amesema, mara baada ya kumalizika kwa mashindano ya kumuenzi baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere yanayofahamika kama Nyerere Cup wanajipanga kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa Mwaka utakaofanyika mwishoni mwa mwezi huu.

Amesema baada ya hapo watakuwa na mashindano ya Klabu bingwa Taifa ambayo yatakuwa ni ya kufunga mwaka yanayotarajiwa kufanyika mwezi wa Desemba mwaka huu.

Kapelela amesema, mashindano ya klabu bingwa Taifa pia yatasaidia kuweza kupata timu bora ya Taifa itakayoweza kushiriki katika mashindano mbalimbali hapo mwakani.