Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mo awashikia bango mashabiki wa Simba

Alhamisi , 14th Mar , 2019

Wakati Simba ikijiandaa na mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi Klabu Bingwa Afrika wikiendi hii, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa klabu hiyo, Mohamed Dewji 'Mo' amezidi kuwajaza mashabiki ili kuisapoti timu yao.

Mo Dewji pamoja na mashabiki wa Simba wakiwa uwanjani

Mchezo huo kati ya Simba na AS Vita Club ya DR Congo unatarajia kupigwa Februari 16 katika Uwanja wa Taifa majira ya saa 1:00 usiku ikiwa ni wiki moja baada ya kutoka kufungwa mabao 2-0 dhidi ya JS Saoura nchini Algeria.

Katika ukurasa wake wa Instagram, Mo ameweka video iliyoambatana na ujumbe unaowataka mashabiki wa Simba kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu yao huku akisisitiza kuwa naye ataungana nao uwanjani.

 

Katika msimamo wa kundi lake, Simba inakamata nafasi ya mwisho ikiwa na pointi 6 baada ya michezo mitano mpaka sasa. Nafasi ya kwanza ikishikiliwa na JS Saoura yenye pointi 8 huku Al Ahly na AS Vita Club zikiwa katika nafasi ya pili na ya tatu.

Mchezo wa Klabu Bingwa Afrika kati ya Simba na JS Saoura

Kwa nafasi ilivyo sasa, kila timu inayo nafasi ya kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano hiyo endapo itafanikiwa kupata ushindi katika mchezo wake wikiendi hii. Ukiachana na mchezo wa Simba na AS Vita Club, pia mchezo mwingine utapigwa nchini Misri ambapo Al Ahly itapambana na JS Saoura kutafuta nafasi hiyo.

Bonyeza hapa chini kutazama zaidi.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi