Jumanne , 19th Mar , 2019

Kiungo wa kimataifa wa Simba kutoka Rwanda, Haruna Niyonzima, ameweka wazi kuwa muda mfupi baada ya kuingia kwenye mchezo dhidi ya AS Vita, aliumia kifundo cha mguu lakini hakutaka kutoka wala kuwaangusha mashabiki.

Haruna Niyonzima (katikati)

Niyonzima ambaye alifanya kazi kubwa ya kusaidia kupatikana kwa bao la ushindi la Simba ambalo liliwapeleka robo fainali ya Ligi ya mabingwa Afrika, amesema siku zote alikuwa na ndoto hiyo hivyo hakutaka kuiacha.

''Niliumia lakini nikajiambia siruhusu hili linikwamishe, sikutaka kuwaangusha mashabiki na kocha kwa kuniamini ukizingatia nilifanya maandalizi ya muda mrefu kwaajili ya siku moja kufanya kitu kama hicho, hivyo nakiri Machi 16, 2019 ilikuwa siku yangu kubwa kwenye soka ngazi ya vilabu'', - Amesema Niyonzima.

Aidha amemshukuru kocha wake Patrick Aussems kwa kumwamini na kumpa dakika chache za kutimiza malengo yake. Niyonzima aliingia kipindi cha pili akichukua nafasi ya Emmanuel Okwi.

Niyonzima amemaliza kwa kusema kuwa baada ya kufika robo fainali sasa anaamini kuwa, wanayo nafasi ya kufika fainali na kikosi chao kinauwezo huo kwa kuzingatia wingi wa mashabiki walionao.

Simba imetinga hatua ya robo fainali Jumamosi Machi 16, 2019 baada ya kuifunga AS Vita mabao 2-1 na kufikisha alama 9 nyuma ya Al Ahly yenye pointi 10 kwenye kundi D. 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

16th march 2019 was a big day for my club career. I thank the coach for puting his trust in me but few minutes after being on the pitch i felt a bad pain on my ankle, but i told myself i wasn't going to let it make me come off. I said i have worked hard on every training session for moments like this. This was a dream i had as a kid to play in the CAF champions league final so nothing will stop me from getting there and i wasn't going to let down Simba sports club fans, millions of Tanzanians and my beloved nation Rwanda. So i told myself i would play with my heart, i didn't need to play with my body when my heart was strong. And now we have the reward of being in CAF champions league quarter finals. Inshallah we will play the final because we have the squad to do that and our fans never ending support. #N8 #footballdoctor

A post shared by niyonzima8 (@niyonzimaharuna) on