Kocha wa Simba Patrick Aussems (kulia) akikumbatiana na mchezaji Miraji Athumani
Aussems amefafanua hilo muda mfupi baada ya EATV & EA Radio Digital kuwasiliana na Mtendaji mkuu wa Simba Senzo Mazingiza na kuthibitisha kuondoka kwa Aussems.
Kupitia mtandao wa Twitter Aussems amesema, 'Ni kweli nililazimika kuondoka kwa siku mbili kwa masuala yangu binafsi, narejea kesho Jumatano tayari kwa maandalizi ya mchezo wetu wa ligi kuu wikiendi hii dhidi ya Ruvu Shooting'.
I had to leave 2 days for personal reasons. I'll be back tomorrow to prepare our match against Ruvu and get 3 more points ... pic.twitter.com/pVdR2gUQNc
— Patrick Aussems (@PatrickAussems) November 19, 2019
Aussems pia amesema kuwa ana imani katika mchezo huo wataendelea kuvuna pointi tatu muhimu. Simba kwasasa inaongoza msimamo wa ligi ikiwa na pointi 22 kwenye mechi 9.