Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Polisi TZ yamrejesha Zahera Ligi kuu

Ijumaa , 2nd Dec , 2022

Aliyewahi kuwa kocha wa zamani wa Yanga, Mwinyi Zahera raia wa Congo DR amejiunga na klabu ya Polisi Tanzania ya mkoani Kilimanjaro kuwa kocha mkuu baada ya kufikia makubaliano na uongozi wa timu hiyo.

Zahera ambaye alikuwa mkurugenzi wa kukuza soka la vijana Yanga, amejiunga na timu hiyo leo akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Joslin Bipfubusa raia wa Burundi ambaye mkataba wake ulisitishwa Oktoba 26, 2022 kutokana na mwenendo mbaya wa matokeo, miezi mitatu tangu ajiunge nayo Julai 26.

Ikiwa chini ya Mrundi huyo, Polisi Tanzania ilicheza mechi tisa ikiambulia pointi tano tu baada ya kushinda moja, sare mbili na kufungwa sita, ambapo alitimuliwa baada ya kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Tanzania Prisons.

Kwa mujibu wa taarifa kwa umma ya klabu hiyo ambayo imechapishwa kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii, makubaliano hayo yamefikiwa leo Desemba 2, 2022 mkoani Kilimanjaro baada ya mazungumzo ya muda mrefu na tahmini ya kina ya kuhitaji kufanya vizuri.

Taarifa hiyo ambayo imetolewa Afisa habari wa klabu hiyo, Frank Lukwaro imewaomba mashabiki na wadau kumpa ushirikiano kocha huyo katika kuliongoza benchi la ufundi.

"Klabu ya Polisi Tanzania inapenda kuujulisha umma na mashabiki wake  kuwa imefikia makubaliano na ndugu Mwinyi Zahera kuwa kocha Mkuu wa timu yetu,"

"Makubaliano na kocha Zahera yamefikiwa leo (Ijumaa) mkoani Kilimanjaro baada ya mazungumzo ya muda mrefu pamoja na tathmini ya kina kwa lengo la kufanya vizuri. Tunawaomba mashabiki na wadau wote kumpa ushirikiano Kocha Zahera katika majukumu yake," imesema taarifa hiyo.

Baada ya kuondolewa Bipfubusa, Polisi Tanzania ilikuwa chini ya Kocha John Tamba ambaye ameiongoza katika michezo mitano ya Ligi Kuu akishinda mmoja dhisi ya Ihefu, sare na Dodoma Jiji na kupoteza dhidi ya Singida Big Stars, Mtibwa Sugar na Simba.

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita