Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rekodi zilizowekwa mchezo wa Uefa Super Cup

Alhamisi , 16th Aug , 2018

Baada ya Atletico Madrid kufanikiwa kuwazamisha mahasimu wao katika mji wa Madrid, Real Madrid kwa mabao 4-2 usiku wa jana. Huu hapa ni mkusanyiko wa rekodi mbalimbali zilizowekwa katika mchezo huo.

Timu ya Atletico Madrid wakishangilia.

Kocha wa Atletico Madrid, Diego Simeone ameweka rekodi ya kipekee katika klabu ya Atletico Madrid baada ya ushindi wa taji la UEFA Super Cup, ikiwa ni msimu wake wa saba tangu ajiunge na klabu hiyo.

Kocha huyo machachari awapo uwanjani, ameweka rekodi ya kuwa kocha mwenye mafanikio kuliko wote waliopita katika klabu hiyo, akiwa ameisimamia timu hiyo jumla ya michezo 382 na michezo 236 kati ya hiyo akishinda na kufanikiwa kushinda makombe saba, ameipiku rekodi ya kocha Luis Aragones aliyeshinda makombe sita.

Rekodi nyingine ya kocha wa Real Madrid, Julen Lopetegui ambaye ameweka rekodi ya kuwa kocha wa kwanza kupoteza mchezo wake wa kwanza wa kimashindano tangu Bernd Schuster alipofanya hivyo mwaka 2007.

Katika mchezo huo pia, Lopetegui ameweka rekodi ya kuwa kocha wa kwanza kufungwa mabao manne au zaidi katika mchezo wake wa kwanza wa mashindano tangu Michael Keeping alipofanya hivyo miaka 60 iliyopita alipofungwa na Celta Vigo.

Tangu mwaka 2009 mpaka 2018 timu kutoka Hispania ndizo zilizotwaa taji la Uefa Super Cup isipokuwa mwaka 2013 ambapo Bayern Munich ndiyo ilitwaa taji hilo, timu hizo za Hispania zimetwaa mara tatu kila moja. Barcelona imetwaa mwaka (2009, 2011, 2015), Atletico Madrid imetwaa mwaka (2010, 2012, 2018) na Real Madrid imetwaa mwaka (2014, 2016, 2017).

Goli la kwanza la Diego Costa nalo limengia katika rekodi ya kuwa goli la mapema zaidi katika historia ya mchezo wa Uefa Super Cup, akitumia sekunde 49 pekee kufunga bao hilo.

Klabu ya Atletico madrid imefikia rekodi ya klabu ya Liverpool ya kutwaa taji hilo mara tatu, ambapo imebeba mwaka 2010 waliifunga Inter Milan, 2012 waliifunga Chelsea na 2018 wameifunga Real madrid.

HABARI ZAIDI

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria