Jumapili , 10th Dec , 2017

Kocha wa Manchester City Pep Guardiola, amesema atastaafu kufundisha soka endapo kitafika kipindi ambacho timu atakayokuwa anaifundisha itashindwa kucheza mfumo wake wa kumiliki mpira yaani (TIKTAKA).

Guardiola ameyasema hayo kwenye mkutano na wanahabari kuelekea mchezo wa leo wa ligi kuu ya EPL dhidi ya mahasimu wao Manchester United. Alipoulizwa atafanya nini endapo aina ya soka analofundisha halitafanya kazi, amejibu, “nitastaafu”.

"Kama hilo litatokea, nitastaafu kwa sababu sitajisikia vizuri kuona mpira hauchezwi vizuri”, ameongeza kocha huyo wa zamani wa Barcelona na Bayern Munich.

Mtaalam huyo wa ufundi raia wa Hispania amesisitiza kuwa anatamani kuona mpira ukichezwa zaidi kuliko aina nyingine ya mbinu hivyo hawezi kuendelea kufunisha wakati kitu anachokifurahia hakipo tena.

“Tangu mchezo wangu wa kwanza na timu B ya Barcelona nilifundishwa kucheza soka la kuvutia hadi naanza kufundisha soka timu B ya Barcelona nilifundisha ‘TIKTAK’ na nilifanya hivyo na timu ya wakubwa na timu zingine nilizofundisha”, amemaliza Guardiola.