Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Salah na mfungo

Ijumaa , 25th Mei , 2018

Daktari wa timu ya Liverpool, Ruben Pons amesema kwamba mshambuliaji Mohamed Salah hatashiriki mfungo wa mwezi wa Ramadhan kwa siku mbili kuelekea mchezo wa fainali wa klabu bingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid.

Daktari huyo amesema hayo leo Mei 25, 2018 wakati akihojiwa na kituo cha radio Cadena SER na kuongeza kuwa katika siku ya Ijumaaa na Jumamosi mchezaji huyo hatashiriki mfungo wa Ramadhan na haitakuwa na madhara yoyote kwa mchezaji huyo.

Taarifa hiyo inakuja baada ya kuenea uvumi kwamba mshambuliaji huyo ataendelea na mfungo wa Ramadhan hata katika siku ya mchezo wa fainali dhidi ya Real Madrid.

Mshambuliaji huyo raia wa Misri ambaye ni muumini wa dini ya kiislamu amekuwa na mafanikio katika klabu ya Liverpool baada ya kufanikiwa kupachika magoli 44 katika michuano yote msimu huu.

Katika kipindi cha mwezi Mtukufu wa Ramadhan waumini wa dini ya kiislamu wanapaswa kufunga kula na kunywa katika kipindi cha mchana mpaka jioni, hivyo ilipekea kuweka shaka kwa wapenzi wa soka kuona Salah atashiriki vipi mchezo wa fainali akiwa katika mfungo.

Liverpool na Real Madrid zitakutana kesho Mei 26, 2018 katika mchezo wa fainali wa ligi ya mabingwa ulaya katika mji wa Kiev nchini Ukraine.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala