Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sekunde 149 zaipeleka PSG nusu fainali

Alhamisi , 13th Aug , 2020

Klabu ya PSG ya Ufaransa imekata tiketi ya kucheza hatua ya nusu fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya UEFA Champions League kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1995.

Wachezaji wa PSG wakishangilia baada ya kufunga bao la pili na la ushindi dhidi ya Atalanta kwenye mchezo wa robo fainali ya ligi ya mabingwa ulaya wakiibuka na ushindi wa mabao 2-1

PSG chini ya kocha Thomas Tuchels ilifunga mabao mawili katika dakika za lala salama na kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wa robo fainali dhidi ya Atalanta BC ya Italia. Atalanta walikuwa wa kwanza kupata bao kipindi cha kwanza dakika ya 27 bao ambalo lilifungwa na Mario Pasalic ambalo lilikuwa ni mbao lake la 12 msimu huu kwenye michuano yote.

Mabao mawili ya PSG yalifungwa ndani ya Sekunde 149, Marquinhos aliisawazishia PSG dakika ya 89 na sekunde 35 na Choupo-Moting akafunga bao la ushindi katika dakika ya pili na sekunde 4  ndani ya dakika tatu za nyongeza zilizokuwa zimeongezwa na mwamuzi Anthony Taylor. hivyo PSG walifunga mabao hayo ndani ya sekunde 149.

Mabingwa hao wa ufaransa watacheza nusu fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya kwa mara ya kwanza baada ya kipindi cha miaka 25. mara ya mwisho PSG kucheza mchezo wa nusu fainali ya michuano hii ilikuwa msimu wa 1994-95 chini ya kocha Luis Fernandez, ambapo waliminjyana na Ac Milan na walitolewa kwa kufungwa jumla ya mabao 3-0 kwenye mchezo wa mikondo miwili.

Katika Hatua ya nusu Fainali PSG watacheza na mshindi wa mchezo mwingine wa robo fainali kati ya RB Leipzing na Atletico Madrid itakaochezwa usiku wa leo.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao