Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serena atwaa taji la Wimbledon kwa rekodi mpya

Jumamosi , 9th Jul , 2016

Mwanadada raia wa Marekani ambaye ni mchezaji bora namba moja kwa mchezo wa tenisi duniani kwa upande wa wanawake Serena Williams nyota yake imeendelea kung'ara tena katika michuano mikubwa ya tenisi ya Grand Slam akitwaa ubingwa wa Wimbledon.

Mwanadada Serena Willams akishangilia baada ya kushinda fainali ya Wimbledon.

Gwiji wa tenisi upande wa kinadada Serena Williams ameshinda fainali ya michuano ya ubingwa wa michuano mikubwa ya tenisi Grand Slam ya Wimbledon na kuifikia rekodi ya mchezaji Steffi Grafs ya kutwaa Grand Slam 22 kufuatia hii leo kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Wimbledon baada ya kumduwaza Mjerumani Angelique Kelber kwa seti mbili mfululizo za michezo 7-5 na 6-3.

Serena mwenye umri wa miaka [34] ndiye aliyekua bingwa mtetezi wa michuano hiyo na sasa anaweka kibindoni taji la saba [7] la michuano hiyo mikubwa ya tenisi Wimbledon kwa kalenda ya michezo ya tenisi dunia.

Ushindi huo kwa Serena ni kama kulipiza kisasi dhidi ya Kelber kufuatia Mjerumani huyo kumshinda katika fainali ya michuano ya wazi ya Australia Iliyofanyika mapema mwaka huu mjini Melborne nchini Austalia.

Lakini pamoja na Serena Williams kufikia rekodi ya Gwiji wa Ujerumani Graf ya kuwa bingwa wa wakati wote wa michuano ya ubingwa mkubwa ama michuano mikubwa ya tenisi ya Grand Slam kwa mtu mmoja mmoja [singles], bado mchezaji huyo anakuwa nyuma mara mbili kwa mchezaji kiongozi wa muda wote wakutwaa mataji makubwa Margaret Court, ambapo raia huyo wa Australia yeye alishinda mataji 13 kati ya 24 katika michuano hiyo mikubwa wakati huo ikiwa ya ridhaa kabla ya baadaye kubadilika na kuwa ya kulipwa mnamo mwaka 1968.

Fainali nyingine ya mtu mmoja mmoja kwa upande wa wanaume itamkutanisha mwenyeji wa michuano hiyo Mwingereza Andy Murray ambaye ni mchezaji bora namba moja kwa sasa nchini Uingereza kwa upande wa wanaume akicheza fainali ya tatu ya michuano hiyo ambapo yeye atakuwa katika kibarua dhidi ya mchezaji Milos Raonic siku ya jumapili Julai 10 mwaka huu.

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita