Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serengeti Boys yaishushia mvua Shelisheli kwao

Jumamosi , 2nd Jul , 2016

Kikosi cha timu ya taifa ya vijana ya Tanzania waliochini ya umri wa miaka 17 Serengeti Boys hii leo imefanikiwa kuiondosha Shelisheli katika mchezo wa marudiano kuwania tiketi ya kucheza fainali za mataifa ya Afrika kwa vijana AFCON U17

Serengeti Boys wakiwa katika moja ya mazoezi yao jijini Dar es Salaam kabla ya kwenda Shelisheli.

Timu ya taifa ya vijana ya Tanzania chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys imeshinda mabao 6-0 dhidi ya Shelisheli katika mchezo wa marudiano wa raundi ya kwanza kuwania tiketi ya kufuzu kwa fainali za vijana U17 Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Madagascar mchezo uliofanyika jioni ya leo Uwanja wa Stade Linite mjini Victoria.

Kwa matokeo hayo, Serengeti Boys inasonga mbele na kwenda raundi ya Pili na hatua ya mwisho ya mchujo kwa ushindi wa jumla wa mabao 9-0 baada ya wiki iliyopita kushinda 3-0 katika mchezo wa kwanza uliopigwa katika uwanja wa Taifa,jijini Dar es Salaam.

Serengeti Boys sasa itamenyana na Afrika Kusini, ikumbukwe hiyo ni kama marudio ya mchezo wa mwaka jana katika hatua hiyo hiyo, ambayo vijana wa Tanzania walitolewa.

Mashujaa wa Serengeti Boys katika mtanange huo ambao walipachika mabao hayo ya Serengeti hii leo nipamoja na Shaaban Zubeiry akifunga bao dakika ya saba, Mohammed Abdalah dakika ya 49, Hassan Juma ambaye alipachika mabao mawili dakika ya 47 na 75, Issa Makamba yeye akifunga kwa mkwaju wa penati kunako dakika ya 65 na msumali wa mwisho uligongelewa na Yohana Nkomola kunako dakika ya 90 na kufanya ubao wa matangazo kusomeka Serengeti Boys 6 wenyeji Shelisheli 0.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea