Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Sikuitwa Yanga, karaha na fedheha zimezidi"- Muro

Jumanne , 25th Feb , 2020

Aliyewahi kuwa Afisa Habari wa Yanga, ambaye sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro amesema kuwa ameamua kurejea katika klabu hiyo kwa ajili ya kuendeleza mshikamano.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro

Amesema hayo kupitia mkutano ulioitishwa na uongozi wa klabu hiyo ukiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa klabu, Fredrick Mwakalebela, ambapo amesema kuwa amekuja kutoa sapoti yake kuelekea mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Gwambina FC kesho.

"Nimekuja tena Yanga sikuitwa ila karaha na fedheha zimezidi nikaona nije tena tushirikiane. Potelea mbali ukuu wa Wilaya ulinikuta nikiwa Yanga hivyo nimeona nirudi na sijaja kuwa kiongozi ila lazima tuungane na kesho Gwambina hana pakutokea", amesema Jerry Muro.

"Mimi niliachia kijiti kwa kina Antonio Nugaz lakini upande wa Simba mwenzangu kakomalia hapo hapo sijui yeye ndio msukule wa Simba?. Kwetu sisi watu wanabadilika, walio walianza na Mo Dewji tangu akiwa mdogo mpaka leo wanamtegemea yeye tu, sisi wamepita kina Manji na wengine Yanga inasonga tu ndio tofauti yao na sisi", ameongeza.

Kuhusu kocha Mkuu wa Yanga, Luc Eymael, Mkuu huyo wa Wilaya amesema, "na mimi kama mwanachama huru nimwambie kocha tumemvumilia sana, kesho tunataka magoli 7, alitoka Ulaya huko kuja hapa atajua anafanyaje".

Aidha Jerry Muro ametoa wito kwa viongozi wote waliowahi kuhudumu klabuni hapo, kurudi na waendelee kuishi kama zamani, kuanzia kesho itakaposhuka dimbani dhidi ya Gwambina FC.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala