Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba Bingwa mpya kombe la Mapinduzi 2022

Ijumaa , 14th Jan , 2022

Wekundu wa Msimbazi Simba wameibuka kuwa mabingwa wa Michuano ya kombe la Mapinduzi mwaka 2022 baada ya usiku wa jana Januari 13, 2022 kuifunga Azam 1-0 kwenye dimba la Amani, Visiwani Zanzibar.

(Wachezaji wa SImba wakisheherekea Ubingwa wa Mapinduzi mwaka 2022)

Bao la pekee la ushindi la SimbaSC limefungwa na mshambuliaji wake, Meddie Kagere dakika 56 kwa mkwaju wa penalty baada ya mlinda mlango wa Azam FC, Mathias Kigonya kumkanya Pape Ousmane Sakho ndani ya eneo la 18.

Ubingwa huo umewafanya Simba kubeba kombe hilo mara ya nne, kufuta uteja mbele ya Azam FC wa kupoteza fainali mbili mbele ya Wanalamba lamba hao pamoja na kujiuliza vema walipopoteza 2021 mbele ya watani wao, Yanga.

Kamati ya mashindano ya Mapinduzi iliwapa zawadi Simba ya Shilingi milioni 25 taslimu kwa kuwa bingwa huku Makamu Bingwa, klabu ya Azam walipewa kiasi cha shilingi milioni kumi na tano taslimu.

Mbali na zawadi za Jumla, lakini kamati hiyo iliendelea kutoa tuzo binafsi kwa wachezaji waliofanya vema ambapo, tuzo ya mfungaji bora imeenda kwa Meddie Kagere, Kipa bora, Aishi Manula na Mchezaji bora Pape Sakho wote wa Simba SC.

Henock Inonga Baka alichaguliwa kuwa nyota wa mchezo wa fainali hiyo baada ya kuonesha umahiri mkubwa wa kuzuia mashambulizi ya Azam FC kwa washambuliaji Rodgers Kola na Idris Mbombo.

Tuzo ya mchezaji bora chipukizi imeenda kwa winga Tepsi Evans, kiungo bora imeenda kwa Kenneth Muguna, beki bora Daniel Amoah wote kutoka kikosi cha mabingwa wa Kihistoria wa michuano hiyo, Klabu ya Azam.

HABARI ZAIDI

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya