Jumanne , 31st Jan , 2017

Simba SC itaondoka Dar es Salaam mapema Alhamis wiki hii kwenda Songea mkoani Ruvuma kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya wenyeji Majimaji.

Simba SC itaingia kwenye mchezo na Majimaji, ikiwa na kumbukumbu ya kufungwa 1-0 na Azam FC Jumamosi katika mechi nyingine ya ligi hiyo.

Kipigo hicho kiliipunguza kasi ya Simba SC katika mbio za ubingwa na kujikuta wakiwapisha kileleni mabingwa watetezi, Yanga ambao juzi walishinda 2-0 dhidi ya Mwadui FC ya Shinyanga.